Vyakula Vya Kuongeza Hamu Ya Mapenzi.

Pamoja na utamu wake, asali ina nafasi kubwa ya kuongeza hamu ya kujamiiana kwakuwa ina aina zote za madini ya Vitamin B, ambayo ndio yanasaidia sana kuupa mwili nguvu.

Unaweza kula vijiko kadhaa kila siku, wengine huichanganya wakiwa wanaotengeneza keki, kuipaka kwenye mkate au chakula chochote.

Shayiri

Maji ya shayiri asubuhi au jioni yanasaidia kuongeza hamu ya kujamiiana. Shayiri madini ya L-arginine yanayoongeza homoni za testosterone, pia ina wingi wa kundi la Vitamin B. Shayiri huuzwa bei nafuu na ni njia rahisi sana ya kuongeza msukumo wa damu, jambo ambalo hutokea unapofanya mapenzi. Shayiri inapotumiwa kwa muda mrefu inasaidia kupunguza uwezekano wa kupata matatizo ya kusimama kwa uume.

Parachichi

Wataalamu wa masuala ya mapenzi wanasema kuwa parachichi linaingia kwenye kundi hili kwakuwa umbo lake linafananishwa na maumbile ya mwanaume au mikunjo katika mwili wa mwanamke na kwamba ulaini wake na jinsi linavyotoa majimaji huongeza hisia za mapenzi. Yanaweza kuliwa yenyewe au kwa kuchanganywa kwenye vyakula vingine.

Yana kiwango kikubwa cha mafuta na vitamin E vyenye kazi ya kuongeza msukumo wa damu, hivyo kuongeza kiwango cha utengenezwaji wa testosterone. Kama hutaki kutumia parachichi kwa kazi hii, basi litakusaidia kwa kung’arisha ngozi kutokana na madini ya vitamin E.

Mbegu za maboga

Mbegu za maboga zina wingi wa madini ya tyrosine (aina mojawapo ya asidi aina ya amino inayosaidia kuchangamsha mwili). Mbegu hizi pia zina virutubisho vingi vinavyosaidia kuongezeka kwa msukumo wa damu mwenye viungo vya uzazi.

Unaweza kuzioka kwenye oveni, kuzisaga au kula kwa kuzichanganya na vyakula vingine, ikiwamo asali pia – ili kuongeza faida zaidi.

Tikiti

Wataalamu wanasema kuwa watu wengi hawajui jambo moja kuhusu tiketi: kwamba kama ambavyo tiketi linaweza kukata kiu yako kwa wingi wa maji yaliyomo, ndio hivyo hivyo inavyoweza kukusaidia kwenye maswala ya kujamiiana. Utafiti umeonesha kuwa tunda hilo lina kiwango kikubwa cha viambata aina ya citrulline, ambayo ina kazi sawa na dawa aina ya Viagra kwa mwanaume.

Tangawizi
Tangawizi inafanya damu iende kwa kasi jambo linaloweza kusababisha mwili uweze kupata msisimko wa kimapenzi kirahisi sana. Pia inasaidia kuboresha mfumo wa usagaji wa chakula, jambo linalosaidia sana kukufanya ubaki kuwa na hamu ya kufanya mapenzi kama umekula chakula kingi.

Chokleti

Wataalamu wanasema kuwa dawa pekee ya ukweli kwenye maswala ya mapenzi ni cocoa. Cocoa inachochea uzalishaji wa homoni zinazofanya ujisikie vizuri aina ya serotonin na dopamine, na ina kemikali aina ya phenylethylamine, inayotengenezwa kwa wingi kwenye ubongo unapoingia mapenzini. Cocoa inafanya kazi hii hasa inapochanganywa na chokoleti kwakuwa inayeyuka kirahisi na kuleta hamasa ya kimapenzi mdomoni. Kwakuwa chokleti ni nzuri unapoila—na inafanya tujisikie vizuri baada ya kuila—zawadi inayomfanya mtu apate hisisa nzuri siku zote lazima itapendwa.

Source: Udaku