SAIDA KAROLI: “NILITUMIWA SANA BILA KUPATA MAFANIKIO YOYOTE YA KAZI YANGU”.

Saida Karoli anaogopa kugusa hata jani, akidhani
ni nyoka anayetaka kumng’ata
Ni kwasababu licha ya kufanya vizuri kimuziki
miaka kadhaa iliyopita, hakupata chochote na
bado anaishi katika mazingira magumu.
“Niliumizwa kuanzia mwanzo, ni vitu vichache
nilivyovipata, kama mkibahatika waandishi wa
habari wenye makamera na wakija kwangu
watashuti kulingana na nilivyo, wataona
mazingira ninayoishi ndipo watanzania watazidi
kufunguka zaidi,” Saida alimwambia mtangazaji
wa Jembe FM, Natty E.
Kwa sasa Saida Karoli anaishi jijini Mwanza. Hivi
karibuni amerejea tena kwenye midomo ya watu
baada ya Diamond kurudia wimbo wake Salome.
Story By:@Joplus_
Source: Udaku Special Blog.