MH. TEMBA AIKIMBIA KAZI YA WIZARA.

download

Msanii wa Kundi la TMK Wanaume Family, Mh Temba amesema alipata shavu la ajira katika moja ya wizara za serikali lakini akakataa.

Rapper huyo ambaye ana taaluma ya Clearing and Forwarding , ameiambia Bongo5 Ijumaa hii kuwa anaamini hawezi kufanya muziki katika maisha yake yote lakini wakati wake wakuajiriwa bado.

“Hivi karibuni nilipata ajira sehemu fulani lakini nikaona bado muda wake, kwa sababu hata nikiangalia mshahara wenyewe ni wakawaida sana na sasa hivi nimeshakuwa na mambo mengi, kwa hiyo nikakataa,” alisema Temba.

Temba alisema anamini hawezi kufanya muziki katika maisha yake yote hivyo anaamini siku anaweza akaajiriwa.

Story by@Joplus_

Source: Muungwana Blog