eki wa Manchester City Benjamin atauguza jera lake la mguu kwa kipindi cha miezi saba.

Beki wa Manchester City Benjamin atauguza jera lake la mguu kwa kipindi cha miezi saba.

Beki huyo wa kushoto ambaye ni raia wa Ufaransa alipata jeraha katika kipindi cha kwanza cha mechi ya ushindi wa 5-0 siku ya Jumamosi dhidi ya Crystal Palace.

”Mendy atakuwa nje hadi nusu fainali ya kombe la vilabu bingwa kati ya 24-25 Aprili”, alisema meneja Pep Guardiola.

Mendy mwenye umri wa miaka 23 alikuwa beki anayelipwa kiasi kikubwa cha pesa duniani baada ya kujiunga na City kutoka Monaco kwa £52m.

”Habari mbaya jamaa”, Mendy alichapisha katika mtandao wa kijamii.

”Nitajiunga na Injury Fc kwa mkopo kwa miezi kadhaa lakini natumai nitarudi hivi karibuni”.

Siku ya Jumanne, Guardiola aliulizwa iwapo angependa kutafuta beki atakayejaza pengo hilo mnamo mwezi January na kujibu ”totaona Januari”.

story@moodyhamza