Ufafanuzi Wa Nape Nnauye kuhusu taarifa zinazomuhusisha yeye na Kinana

Moja kati ya taarifa zilizosambaa leo katika mitandao ya kijamii ni kuhusiana na Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi CCM Abdularahman Kinana kuwa ataongea na vyombo vya habari saa nne asubuhi ofisi ndogo ya chama cha CCM Lumumba Dar es Salaam.

Taarifa hizo hazikuwa za kweli lakini uvumi ukaendelea kuenezwa kuwa Kinana amekatazwa kuongea na waandishi, taarifa ambazo sio za kweli pia huku ikionekana account fake ya Mbunge wa Mtama ambaye ameondolewa katika uwaziri Nape Nnauye ndio kaandika katika twitter account yake.

Hii akifafanua kuhusu ujumbe uliyoenezwa kuwa kamuandikia Kinana

Nape Nnauye ametumia ukurasa wake rasmi wa twitter kueleza kusikitishwa kwake na watu wanaozusha taarifa hizo zenye lengo la kumchafua kuhusu katibu Mkuu wa CCM Kinana, Nape ameandika kuwa hajaandika taarifa hizo zinazomuhusu Kinana.

Source: Millard ayo