Timbulo Awaponda ma Video Queen

Timbulo amewaambia ma model wanaopiga picha za nusu utupu  waendelee mpaka watakapopata wanachokitaka kupitia picha hizo.

Timbulo amesema, “Naona waendelee tu kukaa uchi kwasababu nahisi ni kitu ambacho kina faida kwa upande wao, lakini mimi kama mimi na jamii tuliyonay sidhani kama ni kitu kizuri. Lakini ndo hivyo maana kila mtu anakitangaza kile kitu ambacho anataka kutangaza na kukiuza na bila shaka kuna wateja kwenye hiyo biashara maana ingekuwa vinginevyo wangekuwa wameshaacha.”

Ameongeza, “So nazidi kuwasisitizia waendelee kukaa uchi maana hakuna namna tena kwa sasa.

Source: Dizzim Online.