Takriban watu wawili wameuawa katika mji mkuu wa Nairobi

Takriban watu wawili wameuawa katika mji mkuu wa Nairobi huku maafisa wa polisi wakikabiliana na wafuasi wa kiongozi wa upinzani Raila Odinga .

Gari moja la maafisa wa polisi pia lilichomwa .

Makundi ya watu yalikusanyika katika uwanja wa ndege kumkaribisha kiongozi huyo amabye alikuwa amerejea kutoka mataifa Marekani.

Raila Odinga alisusia marejeleo ya uchaguzi mkuu wa mwezi Agosti.

Kulikuwa na ripoti za maafisa wa polisi waliorusha vitoa machozi katika gari la Raila Odinga alipokuwa akielekea mjini.

Siku ya Jumatatau Mahakama ya juu nchini Kenya inatarajiwa kutoa uamuzi wake kuhusu uhalali wa uchaguzi wa tarehe 26 Oktoba ambao rais Uhuru Kenyatta alibuka mshindi.

@moodyhamza