Maswali asiyopenda Kuulizwa Barnaba Kwenye Intreview

Mwimbaji wa Bongofleva Barnaba Boy ambaye anadaiwa kuwa na mtoto mwingine tofauti na Steve, mtoto mwenyewe anaitwa Maria na mama yake anaitwa Nasra.

Soudy alipomtafuta Barnaba kuujua ukweli alisema maisha yake sio ya mitandao hata kama ana mtoto au hana hawezi itolea kauli yoyote…

..>>>“Niwe nae nisiwe nae ni Mwanadamu amezaliwa, Soudy acha kunichokonoa sana no comment kila mtu kazaliwa nafikiri vitu vingine vinaendelea hata wewe umezaliwa mimi sitaki kupost vitu vyangu kwenye public, wapo watu wanawezaga hayo mambo siyo mimi, wakipata utasema funguo” – Barnaba

Source: Millard ayo