Faiza Ally Amshukia Mbunge Sugu Tena.


Huwa sipendi kupost mambo haya lakini imenibidi, hizi ni bank slips za ada ya mwisho niliyolipa kwenye shule ya kindergarten aliyokuwa anasoma mwanangu za mwezi wa 5 mwaka huu 2017 ambako alishamaliza . Na mwezi huu wa 9 ilikuwa nimuanzishe shule Feza Nursery pale Mikocheni, lakini from no where mama yake ghafla akanizuia na kusema ahitaji tena nilipe ada na hata kunizuia nisimuone tena Sasha! Na kwamba ana uwezo wa kumpeleka shule anayotaka yeye na ndio akampeleka huko Hazina International, ambako pia hata hivyo nilishaanza kuwasiliana na uongozi ili niendelee tu kulipa ada hata kama nimepigwa marufuku kumuona mwanangu bila sababu… # Hivi kama ni nyie mngefanyaje ? Na nyie mnaotukana ovyo mitandaoni bila kuwa na ukweli mnaoujua tafadhali sana naomba hebu kwanza KABILIANENI NA HALI ZENU kwenye maisha… Asanteni

 

FAIZA ALLY:
We baba mjing* lol angalieni risiti za mwaka gani na sasha alianza kusoma lini ?
Ka***mbe mbele na sita kuacha mpaka unyooke ! Mnafki mkubwa ! Toa hata risiti 1 tu ya mwaka 2016 …. zote za mwaka 2017 Tena muhula wa mwisho ! Una haya ada term 2 ku prove kwa watu… wewe na wa p*mbavu wenzie wana kujaz k*ambeni mbele ukweli unaujua kwenye nafsi yako !
Naona umeona aibu mtoto mdogo kama Diamond anavyoweza kuwa reaponsible na watoto pamoja na ujinga wote unaoendelea HAYA NA AIBU ikakushika kuona kuna watoto uliowazidi umri wanakuzidi akili ukajihisi hapa watu watashtuka hapa wataniona mimi bwege maana huyu Diamond kama kavua nguo mababa loosers wote, mbona siku zote ulikuwa hujitetei!? Nimeanza kulalamika leo mimi!? Eti leo huyo unaonesha risiti mbili tu ambazo hata mimi niliwahi kuzipost humuhumu maana nilishtuka, Aibu imekushika, asante Diamond kwa kutushtulia mapunga zeze kama haya.. sasa tufanye kitu kimoja we si unataka kumpeleka Feza, mbele ya watanzania leo NAKUKABIDHI HUYO HAPO njoo umpeleke tuone kama utaweza, na nakukabidhi mbele za watu sababu huongei na mimi na wala hutaki kuwasiliana na mimi juu ya maendeleo ya mtoto na mimi sina shida na hilo sababu siwezi lazimisha mtu aelewe umuhimu wa baba na mama kuwasiliana juu ya mtoto kwa maendeleo yake (mtoto) nenda kalipe Feza uone kama atagoma kusoma, ila leo NIMEKUDHARAU ZAIDI nilijua we ni mgumu ila sikuwahi kufahamu kuwa kumbe unajua kwamba UNACHOKIFANYA KIBAYA deep down na ndiomana leo umedhihirisha kwa kujitetea uongo, unajitetea nini kama unayoyafanya ni sawa!? We si unaona sahihi kutojua hata mtoto anaishije, hebu sema basi hata mara ya mwisho ni mwaka gani kuona hata tigo pesa yako tu ya hata elfu hamsini, naachaje kuwa na uchungu, nalisha, nasomesha, navalisha na hata comfort kwa mtoto ni mimi maana hata kuongea nae tu umegoma, kweli leo unathubutu kutoa risiti zako za muhula eti kujionesha unahudumia mtoto!??? Aisee umenishtua sana, umenitoka zaidi joseph, we ni m*uaji, ila sikushangai umeweweseka na Diamond mtoto mdogo kakuvua nguo we mtu mzima na mizigo yako kwenye suruali.
Nilishawahi kuomba kuweka suluhu hadi na mwanamke wako ili tuwe na amani na mtoto apate amani zaidi kimalezi nikadharauliwa, jiulize Ni mara ngapi nimehangaika kuomba tukae chini tuongee kama wazazi tusolve angalau uweze kuwa kwenye maisha ya Sasha na ukakataa!? Nimemfata rafiki yako Mungai kuongea nae tuweze kukutana kwa ajili ya mtoto uligoma, nimefunga safari hadi Zanzibar mimi kwenda kwa Baba yako wa hiyari unaemuheshimu kuomba tukae chini ajenda ikiwa mtoto tu na ukagoma, hata simu yangu unasema huwezi kupiga wala kutaka kuwasiliana na mimi matokeo unamnyima haki mwanao, hivi kweli juhudi zote hizo mimi leo unathubutu kusema nimekukatalia mtoto!!? Kilichotokea ulimtaka Sasha aje mbeya na ukamtuma mtu aje kukuwakilisha huku ukisisitiza hutaki kabisa kuongea na mimi, kama mzazi na MWANAMKE naruhusu vipi mwanangu aende sehemu ambayo ntashindwa hata kumpigia baba yake kumuuliza tu vipi anaendeleaje, hata akiumwa hutaweza kuniambia sababu eti hutaki kabisa kuongea na mimi, hilo ndio la kusema nilikataza mtoto asije, ni dharau kiasi gani kupigia mtu hata asieishi na mimi kumwambia unataka aniambie anaomba mtoto aje, unajionaje labda, watu wana jinsi wanavyonitafsiri kutokana na maisha yangu mengine lakini laiti kama wangejua naapa hakuna ambae angekutazama mara mbili, na hata kama kweli niliwahi kukosa ama nakukosea, sasa mtoto wako vinamuhusu nini!? Tufanye nisingekuwa na uwezo wa kuhudumia inamana ungemuacha awe chokoraa kama mwanao wa kwanza ambae ni fundi garage uliemtupaga wala hujui alipo uliemkimbizia kijijini kuogopa aibu ya kufatwafatwa kuulizwa na vyombo vya habari, usinijali mimi ila muogope hata MUNGU basi, ogopa kudanganya, unajua mimi sidanganyi na unajua ukweli, nna risiti sio chini ya saba, na bado maisha ya kila siku, kula, nguo kuvaa, michezo bata nnalompa mwanao sijajumlisha hata kimoja leo we risiti mbili unajiita mwanaume zinakusimamisha shingo kweli!?? Hujiskii hata vibaya ukimuona mwanao amependeza labda, mtoto mzuri ana maendeleo mazuri nafsi haikusuti ama hata kuona tu huyu kiumbe anakua na atayajua hayo mambo yako, hauniadhibu mimi unamuadhibu mwanao na zaidi haunikomoi mimi unajikomoa mwenyewe.

Source: Udaku.