Ni nini maana ya Uislamu?

Kilugha lina maana ya njia au mwenendo . Katika kulitafsiri neno hili na jinsi linavyotumika kisheria itabidi tuliangalie katika hali tofauti na maana zake ili tuweze kupambanua wakati linapotumika linakusudiwa kitu gani.

SUNNAH KWA MTAZAMO WA KIHADITHI

Ni kila kilichopokelewa kutoka kwa Mtume Salla llahu ‘Alayhi Wasallaam katika kauli ,vitendo , iqrari , sifa ya kimaumbile , sifa ya kitabia tokea kabla ya kupewa utume mpaka baada ya kupewa utume.

Na katika maana hii neno sunnah na hadithi ni sawasawa

SUNNAH KWA MTAZAMO WA KISHERIA

Ni kila aliloliamrisha Mtume (Salla llahu ‘Alayhi Wasallam) au alilolikataza au alilolipendekeza katika kauli na vitendo na iqrari- [kitendo cha Mtume(Salla llahu ‘Alayhi Wasallam) kumuona mtu akitenda jambo na asitoe maelekezo yoyote ya kukemea au kukataza] Na jambo hili kutumika kama dalili katika hukumu ya kisheria.

SUNNAH KWA MTAZAMO WA KIFIQH

Ni kila jambo ambalo limethibiti kwa Mtume Salla llahu ‘Alayhi Wasallam lakini halipo katika hukumu ya fardhi wala wajibu.

story@moodyhamza