Baada ya Chibu Perfume… Alikiba atangaza bidhaa atazoleta

Habari njema za Mastaa wa bongo kutengeneza njia za kujiongezea kipato zaidi kwa kutengeneza bidhaa zenye majina yao zinaendelea kuongezeka ambapo leo ni zamu ya Alikiba.

Zikiwa zimepita wiki mbili toka Mwimbaji mwingine staa wa Bongofleva Diamond Platnumz kuzindua Perfume yake, leo May 11, 2017 kupitia 255 ya XXL Mwimbaji staa wa ‘aje’ Alikiba ameweka wazi kuwa moja ya mipango yake ni kutoa mavazi aina ya jeans, miwani, viatu na vinywaji vya energy vyenye jina lake.

Alikiba amesema kuwa hiyo ni mipango mizito na hatarajii kuifanya kiholela kwani hata mwanzo alifanya kama promotion lakini sasa hivi hayupo tayari kuikosea serikali na amejipanga kufungua na duka ili watu wake waweze kupata kwa urahisi.

“AK ni Brand ya Alikiba nashukuru imekuwa kubwa watu wanavaa lakini pia ipo na ya King Kiba nayo ni brand yangu na zipo official kabisa na kazi zitakapoanza watapata product zote’ – Alikiba

“Kuna Malengo makubwa sana tumeyaweka lakini siwezi kusema sasa hivi ila kuna Jeans Viatu na Glasses tayari zishatoka soon wataziona maana hizi zitakuwa za kwanza sababu tayari zishatoka na kuna energy drink” – Alikiba

Source: Millard Ayo