Watu wengi wamekuwa wakisumbuliwa na maradhi ya Fangasi, za miguuni ama sehemu za siri ..

IFAHAMU TIBA YA FANGASI SUGU YA NJE.

Watu wengi wamekuwa wakisumbuliwa na maradhi ya Fangasi, za miguuni ama sehemu za siri zenye kuambatana na kero kubwa kama kuwashwa sehemu hzo za siri ama miguu kutoa harufu pindi avuapo viatu.

Na wengi wao wamehangaika madawa mbalimbali pasina mafanikio yoyote.

Ifuatayo ni dawa mujarabu ya fangasi sugu ya nje:

DAWA:
1. Nyongo ya Ng’ombe.
2. Halimiti (Sulphur ya njano)

MATIBABU.

1. Changanya nyongo ya Ng’ombe na Salfa ya njano kiasi kinachowiana upate mchanganyiko mzuri.

2. Uwe unajipaka sehemu husika kila siku muda wa kulala.

3. Hakikisha unaosha eneo la ugonjwa na kulikausha vizuri kabla hujapaka dawa.

Kwa Maelezo zaidi tuwasiliane.
UGONJWA UKIZIDI MUONE DAKTARI.

story@moodyhamza