“Kuwacontrol wanawake ni ngumu sana” – Lamar

Ayo TV Entertainment ilifanya exclusive interview na producer Lamar kutokea Fishcrab ambapo ilimuuliza sababu iliyopelekea kuvunjika kwa kundi la Shostiz ambalo lilikuwa linaundwa na wasanii watatu wa kike akiwemo mwanadada Menina ambapo alisema sababu kubwa ya kuvunjika kwa kundi hilo ni ugumu aliokuwa anaupata katika kuliongoza kundi la muziki lenye wanamuziki wanawake tupu.

“Unajua kuwacontrol wanawake ni ngumu sana. Unakuta kila mtu anaamka akiwa kwenye mood zake. Labda tumepanga kushoot halafu unakuta huyu hayupo kwenye mood nzuri. Ilikuwa ni ngumu kwangu pia walivyotengana na kila mmoja kuolewa, so ikawa ngumu kwa kundi kuendelea.” – Lamar.

Nilimuuliza pia kuhusu msanii Geez Mabovu aliyefariki mwaka 2014, vipi kazi zake ambazo hazijatoka na kama ana mpango wa kuziachia.

Source: Millard ayo