Chameleone na Bob Wine Waongea Yao Kwenye Msiba

 

Watu mbalimbali wakiwemo mastaa wa muziki wa Uganda walikuwa ni sehemu ya waliohudhuria mazishi ya aliyekuwa Mfanyabiashara maarufu nchini humo Ivan Don ambaye amezikwa May 30, 2017 kwao Kampala.

Miongoni mwa mastaa wa Muziki kutoka Uganda ambao Ayo TV na millardayo.com imekutana nao kwenye msiba huo ni Jose Chameleon na Bobi Wine ambao hawakusita kueleza hisia zao juu ya msiba huo.

“Kiukweli Ivan alikuwa rafiki yangu na mimi kama rafiki yake nimeumia sana lakini hatuna chochote cha kufanya kuliko kumuombea Mungu.” – Jose Chameleon.

Source: Millard ayo