Baraka the Prince aelezea ugumu wa kuachia kazi mpya kipindi hiki

Kwasasa Siasa imechukuanafasi kubwa kwenye masikio ya watu hivyo kuweka ugumu kwa wasanii wanaoachia kazi zao mpya kipindi hiki, Braka da Prince ni mmoja ya walioachia kazi mpya kipindi hiki.

Baraka da Prince ambaye ameachia audio na video mpya ya wimbo wake wa “Acha niende” amefunguka ugumu aliokumbana nao kipindi hiki alipohojiwa na Harakati za Bongo

“Changamoto kubwa ni watu wanaconcertrate sana kwenye mambo yanaoyendelea kwenye ma’social network kuhusu serikali, sasa kuna mashabiki wetu wanakua wanapoteza muda wao mwingi huko, lakini mimi naamini sana kazi yangu  na nyimbo nzuri inadumu” Baraka alifunguka.

Aidha Baraka amesema mambo yanayoendelea yanapita na kazi nzuri inadumu kwahiyo hana hofu na kazi yake.

Source: Teen tz