WANAOSHANGAA Tanzania Kuomba Afrika Kusini Msaada Huenda Wakawa Hawajui Haya

Sasa mnashangaa nini Tanzania kuomba Afrika ya Kusini.
Hivi mmesahau jinsi tulivyowasaidia hawa tena buree.
Tuliwapa ofisi.

Tuliwalipa mishahara.

Tukatoa jeshi letu kuwafundisha mapigano.

Tuliwapa silaha za kivita , magari ,vifaru.

Walikula ng’ombe wetu na kuku wetu.

Wakaoa na kuzaa na dada zetu.

Kiufupi Uhuru wao tumeutengeneza sisi Tanzania.

Tulitoa fedha za Watanzania kwa ajili ya ukombozi wa ndugu zao wa Afrika ya Kusini.

Leo isiwe nongwa , acheni watulipe fadhila kwa wema tuliowatendea.
Mahusiano na yadumu.

Afrika ni moja na itabakia kua moja .

Source: Udaku