Kwa wanaosema Alikiba hapost show za tour zake iwafikie hii

Kila siku ni kawaida yangu kukusogezea mambo mbalimbali kutoka kwenye mitandao ya kijamii kuhusu muziki, siasa, burudani na michezo hasa kutoka kwa mastaa wa ndani na nje ya Tanzania.

Mashabiki wengi wa muziki wa Bongofleva hasa wanaomkubali staa Alikiba wamekuwa wakihoji juu ya staa huyo kutopost picha na video za show zake anazoendelea kuzifanya sehemu mbalimbali duniani, sasa leo April 26, 2017 kupitia Ayo TV na millardayo.com mashabiki hao watafahamu zaidi kuhusu hilo.

Source: Millard ayo