DAVIDO AMPOKONYA DIAMOND KITI CHA FOLLOWERS INSTAGRAM.

Msanii wa Nigeria, Davido amefanikiwa kufikisha follower milioni 2.9 kwenye mtandao wake wa Instagram na kuwa muimbaji wa kwanza Afrika kuwa na followers wengi zaidi kwenye mtandao huo.

Mpaka wiki iliyopita nafasi hiyo ilikuwa ikishikiliwa na msanii wa Tanzania, Diamond Platnumz mwenye follower 2.7 milioni kwenye mtandao huo lakini kwa sasa atashika nafasi ya pili.

Mpinzani wa karibu wa Davido, Wizkid ana followers milioni 2.5.

Waimbaji wengine wenye followers zaidi ya milioni moja ni:

Don Jazzy 2.2 milioni
Tiwa Savage 2.2 milioni
Vanessa Mdee 1.8 milioni
Alikiba 1.4 milioni
Yemi Alade 1.2 milioni

Story by:@Joplus_

Source: Udaku Special Blog