Kundi la Hip Hop lililoanzishwa miaka ya 2005 jijini Arusha, Tanzania. Kundi hili awali liliundwa na wasanii wanne: Lord Eyez, G Nako, Bou Nako, na Ibra Da Hustler. Walijipatia umaarufu kwa staili yao ya 'hardcore' inayoelezea maisha halisi ya mtaani.Jina "Nako 2 Nako" linatokana na maneno ya kiingereza "Fist to fist" (ngumi kwa ngumi), likiwa na maana ya kupambana, na lilianzia katika kambi ya mazoezi ya viungo (dojo) walipokuwa wakikutana.