Sound Engineer wa Cardi B ampigia Magoti Beyonce

Sound Engineer wa Cardi B, Ashby The Mix Engineer, amemuomba radhi Beyonce na mashabiki wake baada ya kuvujisha taarifa za kuwa hitmaker huyo wa ‘Bodak Yellow’ amerekodi wimbo na Queen Bey.

Beyonce anafahamika kwa kufanya kazi zake kwa usiri mkubwa hivyo baada ya habari hizo kuvuja mashabiki wake walimshambulia vikali Ashby na hivyo ameamua kuomba radhi.

Ametumia Snapchat kusema, “Public apology to Beyonce and all her fans unfortunately Hot New Hip Hop invated my privacy. In everything that I post it’s been nothing but encurancement [sic] to my small IG following that’s trying to grind like me in this tough business.”

“I cannot turn back the hands of time so at least this a life lesson I’ve learned on my behalf and all I can do is move forward,” ameongeza.

Source: Dizzim Online.