OMOG afukuzwe’, ‘Omog abaki’, ‘Omog hatufai’, ‘Omog ni tatizo’, ‘timu hazichezi vizuri tatizo ni Omog’.
Hizo ni baadhi ya kauli ambazo zimekuwa zikitawala kwenye vyombo vya habari, mitandaoni, kwenye vijiwe na kwingine kote ambapo kuna mazungumzo kuhusu Klabu ya Simba.
Simba ipo katika nafasi ya nne ikiwa imezidiwa pointi mbili na Mtibwa Sugar ambayo inashika usukani katika Ligi Kuu Bara, pointi za Simba ni sawa na zile za wapinzani wao wa jadi, Yanga, wote wakiwa wameshinda michezo miwili na kupata sare mbili.
Ubingwa unawaniwa na timu zote lakini Simba kunaweza kuwa na presha kubwa zaidi ya timu nyingine zote kutokana na mazingira halisi ya timu hiyo hasa ni kutokana na kutumia kiwango kikubwa cha fedha katika usajili, pili ni kiu ya kuutaka ubingwa wa ligi hiyo baada ya Yanga kutawala kwa miaka kadhaa.
Omog amewahi kuipa ubingwa Azam FC, pia ndiye aliyeiwezesha Simba kupata nafasi ya kurejea katika michuano ya kimataifa, kwa wasifu wake katika soka la Afrika sina shaka na uwezo wake wa kufundisha hasa ukizingatia aina ya mazingira ambayo anafundishia.
story@moodyhamza