Mwarabu Body Guard Wa Diamond Aeleza Ya Moyoni.

Mimi ni shabiki mkubwa wa diamond platnumz.. na wcb kwa ujumla..

Kuna mtu hasikiki sana anaitwa mwarab fighter. huyu jamaa anajua sana kutimiza majukumu yake..

Niliangalia video leo akiwa anampokea zari.. jinsi anavyomuongoza kuhakikisha anakuwa safe… mpaka raha.. kuna muda zari anashangaa shangaa mwarab anamshtua tembea mama…

Hata diamond kipindi anazindua karanga mwarab anavyohakikisha bosi wake yupo safe mpaka raha yaani..

Jamaa ni mtu mzima na anajua sana anachofanya.. anatimiza majukumu kiutu uzima kabisa..

Hongera sana mwarab fighter kwa kufanya kazi yako kwa ubora.. na hongera sana diamond kwa kutoa ajira kwake..

Swali hivi hapatagi mzuka wa kiume.. maana kuna picha wapo dubai diamond na zari wamepakatana.. huku mwarabu yupo pembeni analinda.. najiuliza mashine haipataki ukakasi mazingira hayo kulinda wapendanao…

Jamaa ni jembe sana.

Najua diamond unamtembeza sana duniani.. kila unapoenda nae anaenda… safi sana kwa upendo wako… usisite kuhakikisha unamlipa vizuri na kumshauri pia awekeze ili watoto wake nae wajue baba yao alikuwa ni jembe…. asisishie kuendesha magari tu

Source: Udaku.