Mr Nice Azushiwa Janga.


Msanii  mkongwe wa muziki, Mr Nice ambaye kwa sasa anaishi nchini Kenya amekuwa alizushiwa mambo mabaya na vyombo vya habari kila kukicha ambapo Jumatatu hii katika sherehe za kuapishwa kwa Sonko amezushiwa kitu kingine.

Muimbaji huyo katika show hiyo alidaiwa kuibiwa baadhi ya vitu baada ya kuvamiwa na mashabiki kitu ambacho amekanusha.

“Waandishi vilaza mnapenda kurukia sana hata msilolijua mimi katika show ya kuapishwa Sonko leo sijaibiwa na mtu yoyote,” Mr Nice aliandika Facebook “Kifupi ni kwamba mashabiki waling’ang’ana kucheza na mimi na bahati mbaya wakajikuta wamekata cheni zangu na pia leseni yangu ikadondoka nilikuwa nayo kwa mfuko wa koti la suti,”

Aliongeza, “Mkome kabisaaaa kutengeneza ishu za kipumbavu ili muuze vijikaratasi vyenu huko mtaani. Kenya iko sawa na hakuna tatizo lolote kabisaaaaaa na bado 21/8/2017 tuwache rafiki yangu Sonko achape kazi na Nairobi ifaidike naye,”

Miezi miwili iliyopita muimbaji huyo alizushiwa kifo kupitia mitandao ya kijamii.

Source: Udaku.