Mke Wa Roma Mkatoliki Achafukwa.

Msanii Roma amefunguka na kuzungumzia kuhusu wasanii wenzie walivyolichukulia tukio lake la kutekwa akisema baadhi walibeza na kumtaja Nay Wa Mitego ambaye alipost ujume ulioashiria kuwa Roma alipewa hela ingawa alidai ni rafiki yake.

 

Mbali na hiyo, amesema mke wake alichukia kuhusu ishu ya Madee mpaka akampost na kusema kuwa siyo marafiki ingawa anacheka nao lakini siyo marafiki.

 

Aidha, Roma hakusita kuzungumzia baadhi ya wasanii waliokwenda kumuona alipopata matatizo akisema hawafiki 10.

Hili tukio limenifunza mengi, mkikaa kifamilia na mkeo anakuambia kuna fulani ni rafiki yako mbona hakuja? Tukio lenyewe limewafanya watu kuniogopa. Nimekutana na Madee mwenyewe ndio hizo ananizingua, ananambia nije nikucheki na mimi nitekwe? Hata ile ya Madee, wife ana-mind anasema washikaji gani ukipata matatizo hawaji kukuona? Hata ukiangalia lile tatizo wachache ndio walikuja kuniona hawazidi hata kumi.” – Roma Mkatoliki

Source: Millard ayo