Marekani Yaisifu Tanzania

Taifa la Tanzania limetajwa kuwa kivutio kizuri cha safari za watalii barani Afrika kulingana na mtandao wa SafaricBookings.com ambao ndio mtandao mkubwa wa ukuzaji wa safari za Afrika.

Mtandao huo ulifanya tathmini ya zaidi ya wataalam 2500 na wale walioshiriki katika safari hizo kabla ya kutangaza kuwa Tanzania ndio eneo bora la safari mwaka 2017.

Tathmini hizo ziliandikwa na watalii walioenda safari pamoja na wataalam bingwa wa Afrika.

Mtandao huo unasema kuwa uchanganuzi huo pia ulibaini kwamba Tanzania ilipata umaarufu wake kutokana na idadi ya wanyama mbali mbali.

Watu maarufu katika miezi ya hivi karibuni wamekuwa wakizuru taifa hilo wakitembelea maeneo tofauti ya vivutio vya utalii nchini Tanzania.

Watu hao ni mwanamuziki maarufu Usher Raymond, aliyekuwa mchezaji wa klabu ya Manchester United na Real Madrid David Beckham, aliyekuwa mchezaji wa Liverpool Mamadou Sakho , mchezaji wa Everton Morgan Schneiderlin na nyota wa filamu kutoka Marekani Will Smith na Harrison Ford.

Walitembelea mbuga za Serengeti na mlima kilimanjaro.

Mtandao huo uliitaja Zambia kuwa taifa lenye kivutio kizuri cha misitu huku wataalam wote wakikubaliana kwamba mazingira ya misitu nchini humo mi mazuri zaidi.

Vilevile Zambia pia ilitajwa kuwa taifa lenye maisha bora ya ndege.

Namibia na Kenya zilitajwa kuwa bora katika mandhari mazuri pamoja na ndege waliopo mtawalia.

Source: Udaku