HII NDIYO SABABU INAYOMFANYA ALIKIBA ASIOE.

Alikiba ameitaja sababu iliyomfanya ashindwe kumuoa mwanamke yeyote kati ya watatu aliozaa nao.

Hitmaker huyo wa Lupela alisema kuwa hakupenda kulazimisha iwe hivyo.“Unajua hauwezi kumuoa mtu kama hamuelewani.

“Nia yangu ilikuwa ni kustick na kila mama wa mtoto wangu toka nilipoanza. Lakini mambo yanaenda tofauti, huenda tunapogombana anatafuta mtu mwingine,” anasema Kiba.“Kwahiyo hautakiwi kuforce mapenzi, mimi nataka nikae na mtu ambaye tutaelewana,” ameongeza.

Alikiba ana watoto wawili wa kike, Amiya Kiba, Chamy Kiba na mmoja wa kiume, Sameer Kiba. Wote ni watoto wa mama tofauti.

Story By: @Joplus_

Source: Udaku Special Blog