Graca Machel Amshtaki daktari wa Nelson Mandela

 

Mjane wa aliyekuwa rais wa Afrika Kusini Nelson Mandela Graca Machel, amesema atamshtaki daktari wake bwana Mandela, kutokana na taarifa alizochapisha kwenye kitabu kuhusu siku za mwisho za Mandela.

Daktari huyo Vejay Ramlakan aliongoza kikosi kilichomhudumia Mandela hadi kifo chake Disemba mwaka 2013.

Radio ya taifa nchini Musumbiji ilitangaza taarifa iliyotolewa na wakfu wa Bi Machel ikilaani kitabu hicho vikali.

Bi Machel alisema kuwa kitabu hicho kinakiuka heshima ya bwana Mandela.

Kitabu hicho kimeandika taarifa kuhusu siku za mwisho kabla ya kifo cha Mandela.

Kimetaja kutokuwepo kwa maelewano kati ya madaktari na familia ya Mandela.

Bi Mandela anasema kuwa kitabu hicho kilikiuka siri iliyo kati ya daktari na mgonjwa.

Source: Udaku